Msanii wa filamu Bongo, Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’
MSANII wa filamu Bongo, Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ amejikuta katika wakati mgumu baada ya kutokwa na mabaka mwili mzima
Hivi karibuni, paparazi wetu alimnasa Vai wa Ukweli akiwa nyumbani kwake maeneo ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam ambapo alisema anashukuru Mungu kwani yupo kwenye dozi ya mwezi mzima baada ya kugundulika ana ‘aleji’ hivyo kukatazwa na daktari asile vyakula vyenye ngano na mafuta mengi.
Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ akiwa na bwanake.
“Yaani mbona sasa hivi nina nafuu, mwanzoni nilikuwa nimevimba sana, nilienda Hospitali ya Mwananyamala wamenipa dawa naendelea kuzitumia mpaka mwezi uishe. Unajua nimeshindwa hata kufunga mwezi huu wa Ramadhani kutokana na kuumwa,” alisema Vai wa Ukweli
ISOME NA HII
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment