Wednesday, July 2, 2014

Sio Bongo tu Hata ulaya Yanatokea.MWANAMKE AJIFUNGUA MTAANI JIJINI BIRMINGHAM, UINGEREZA.

Watu wa huduma za afya wakiwa wamemzungushia mashuka ‘mzazi’ huyo.

Mwanamke huyo baada ya kujifungua akiwa amezungukwa na watu waliokuwa wanamhudumia.

Magari ya huduma yakiwa yamefika kumchukua mama na mwanawe katika duka la Primark.

MWANAMKE mmoja ambaye jina lake halikuweza kujulikana mara moja, aliwashangaza wapita njia katika jiji la Birmingham, Uingereza, majuzi baada ya kujifungua mtaani nje ya dula na nguo la Primark.

Mama huyo alijifungua salama-salmin mtoto wa kike baada ya kuzidiwa uchungu akiwa kando ya barabara.  Wapita njia waliokuwa wakipita mtaani majira ya saa nane alasiri walimtafutia gari la wagonjwa, wakamwekea mablanketi chini  na kumzungushia mashuka mama huyo ambaye alikuwa amelala chini ili kumsitiri.

Watu wengi walifikiri kulikuwa na onyesho fulani mtaani hapo, lakini wakagundua ni mama huyo alikuwa amejifungua.  Mama na mtoto walipelekwa Birmingham City Hospital kwa huduma zaidi.

CHANZO: MIRROR


Bonyeza Like hapo juu uwe wa kwanza kupata habari mpya.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top