Wednesday, July 2, 2014

Mwanaume Abakwa Baada ya kupanda lifti ya Gari la mtu asiyemjua.

Mwanaume mmoja amebakwa katika barabara ya daraja lenye shughuli nyingi mjini Newcastle baada ya kukubali kupanda lifti ya mtu asiyemjua.

Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 24 aliingia kwenye gari hilo dogo mapema alfajiri ambapo alifanyiwa kitendo hicho cha ubakaji katika eneo lenye nyasi nyingi karibu na daraja la Redheugh, Newcastle.

Timu ya uchunguzi wa makosa ya ubakaji hivi sasa inaendesha msako wa mtu aliyetekeleza kitendo hicho na kuwataka mashuhuda kujitokeza hadharani.

Afisa upelelezi kutoka mji wa Newcastle, Caroline Ord, amesema hili ni tukio baya zaidi kutendewa kwa kijana huyo ambapo sasa polisi wanafanya kazi bega kwa bega na mtu huyo kuhakikisha wanampata aliyetenda kosa hilo. 


Bonyeza Like hapo juu uwe wa kwanza kupata habari mpya.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top