Monday, July 21, 2014

KATANGAZE!!! DUME LAANDALIWA KEKI NA KUSUTWA MBAYA KISA, UMBEYA.

Keki ya msuto aliyoandaliwa Bw. Sajo.

WERAA! Watu weweee! Dume lililofahamika kwa jina moja la Lusajo au Sajo anayefanya kazi maeneo ya Kijitonyama, Dar jirani na duka la mtangazaji Maimartha Jesse ‘Mai’ amejikuta akitaharuki na kuaibika baada ya kusutwa laivu katikati ya wanawake huku akilishwa keki na kufunguliwa mvinyo kisa umbeya, Ijumaa Wikienda limeshuhudia tukio zima.

9-year-old South African boy marries 62-yr-old woman in South Africa.

Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa eneo la tukio wikiendi iliyopita kabla ya gazeti hili kutua, Maimartha alidaiwa kusuka ishu hiyo huku akiwakaribisha marafiki zake kushuhudia akiwemo Flora Mvungi.


Maimartha akifungua Shampeni.

Ilisemekana kwamba Mai alidai kuwa kilio chake kwa muda mrefu ni kwamba jamaa huyo amekuwa akimfuatafuata na kumwambia mumewe, Raymond Shayo ‘Shaa’ kila jambo analolifanya dukani hapo, ikiwa ni pamoja na kumweleza watu wa kila aina wanaoingia ndani hapo.

“Nilishapata taarifa za Sajo kuwa huwa ananichunguza, sikutaka kuwa na haraka nikaenda naye taratibu bila kumwambia kwani nilikuwa nikimtafutia dawa ya kumkomesha. Leo ndiyo arobaini yake imefika.

Mwanaume aliyesutwa akilishwa keki na Maimartha.

“Nilishika simu ya mume wangu nikakuta SMS za Sajo zikimuomba fedha, ukweli nilichukia sana na nilishangaa kuona kumbe kazi anayoifanya ya kunichunguza analipwa, nikaona sasa ndiyo wakati wa kumkomesha kwani kwa kulipwa kwake ipo siku atatunga hata uongo kwa sababu fedha ni shetani,” alisema.

Lusajo, 'Sajo' akihojiwa na Gea.

Sajo, kabla ya kujua kinachoendelea, alikaribishwa keki na shampeini, akaenda kichwakichwa, alipomaliza kulishwa akaambiwa asome maneno yaliyoandikwa kwenye keki ‘Sajo acha umbeya ndoa  tamu’ ndipo akachanganyikiwa na moja kwa moja msuto ukaanza huku akiulizwa ni kwa nini anamwambia maneno mume wa Mai.

Baadhi ya wadau walioalikwa na Maimartha kumsuta Bw. Sajo kwa umbea.

“Mh! Mimi mbona siyo kweli jamani,”  alisema Sajo na kushindwa kumalizia maneno.
Alipobanwa na wanahabari wetu na Gea Habibu (wa Leo Tena ya Clouds FM) juu ya kuwa na namba ya simu ya mume wa Mai, Sajo alishikwa na kigugumizi na kuondoka ambapo alikimbilia dukani kwake na kujifungia kukwepa aibu kwani siyo tukio la kawaida kwa mwanaume kusutwa kwa umbeya.

Bonyeza Like hapo juu uwe wa kwanza kupata habari mpya. 

 

Excitiment Photos of Students Bash After Finishing Their Exams...!

 

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top