Thursday, February 6, 2014

DUDE kugombea Ubunge 2015 Jimbo la Tabora Mjini;Atachuana na Rage, Stori kamili hapa.


 
Msanii wa maigizo na filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’.
WIMBI la wasanii kuingia kwenye siasa limeendelea kushika kasi ambapo awamu hii msanii wa maigizo na filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ ametangaza kugombea ubunge kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.
 ‘Akistorisha’ na paparazi wetu, Dude alisema kutokana na sanaa kutotoa masilahi ipasavyo, ameamua kuingia kwenye ulingo wa siasa ambapo anatarajia ‘kunyakua’ Jimbo la Tabora Mjini ambalo kwa sasa linaongozwa na Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage.
“Natarajia kugombea ubunge nyumbani kwetu Tabora mjini, niko tayari kuchuana na Rage na kwa sasa  nipo katika maandalizi ikiwemo kuwa karibu na wananchi kwani  wananikubali sana, hivyo natarajia ushindi tu,” alisema Dude.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top