Wednesday, January 1, 2014

Waziri wa Fedha, Dk. William A. Mgimwa (63) amefariki dunia nchini A.Kusini baada ya maradhi ya mda mrefu.


Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa waziri wa fedha amefariki dunia nchini Afrika ya Kusini alikolazwa kwa maradhi yaliyomsumbua mda mrefu.

Mgimwa aliyezaliwa January 20, 1950 alikuwa amelazwa katika hospitali ya Milpark ambayo pia Dk. Sengondo Mvungi. alilazwa kwani hospitali hiyo inaumaarufu wa kusaidia kuwatibu watanzania.



Dk. Mgimwa alikuwa mkufunzi katika Chuo cha Benki mkoani Mwanza, kabla ya kufanikiwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Kalenga, Mkoa wa Iringa, katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.


Tutazidi kukujulisha kila matukio yanayoendelea.
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online