Thursday, November 6, 2014

NDEGE YA RAIS WA CHINA YAHUSISHWA NA WIZI WA PEMBE YA NDOVU.


Ndege ya rais wa China.
Inadaiwa kuwa wanunuzi, raia wa Uchina walinunua maelfu ya kilo za pembe za ndovu nchini Tanzania na kuzitorosha kutoka nchini humo katika ndege ya binafsi ya Rais wa Uchina, Xi Jinping wakati alipozuru bara Afrika. Kulingana na shirika la ujasusi la mazingira lililo na makao yake mjini London.

Pembe hizo zilinunuliwa wiki moja tu kabla ya ziara ya rais huyo wa China kuja nchini tanzania mwaka ulioipita ambapo zilifichwa katika mifuko ya wanadiplomasia ili kutokamatwa.

Shirika hilo pia linadai kwamba wajumbe waliokuwa wakiandamana na Rais Xi walinunua viwango vikubwa vya pembe hizo.

Pembe za ndovu.

Uuzaji wa Pembe za ndovu ulipigwa marufuku mwaka 1989 ili kuwazuia wawindaji haramu kuwaua ndovu.

jjjjjjjjjjjjjjjjjj

HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINi

SOURCE BBC/SWAHILI

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online