Wednesday, November 12, 2014

Breaking News; WATU KADHAA WAFARIKI KATIKA AJALI YA BASI KAHAMA.


Basi la Wibonela wakati likitolewa eneo la tukio.

Wananchi wakishuhudia basi la Wibonela lililopinduka leo asubuhi huko Kahama.

WATU kadhaa wamepoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa asubuhi hii kwenye ajali ya basi la Wibonela lililokuwa likitoka Kahama kwenda Dar lililopinduka eneo la kona ya Phantom, Kahama.

Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi uliopelekea dereva wa basi kushindwa kulimudu lilipofika kwenye kona ya Phantom na kupelekea kuingia mtaroni na kupinduka.

Idadi kamili ya waliopoteza maisha na majeruhi kwenye ajali hiyo bado haijafahamika.

Baadhi ya miili tayari imetolewa katika eneo la ajali huku majeruhi nao wakikimbizwa kwenye Hospitali ya Wilaya Kahama kwa matibabu.

MKE ANAYEISHI NA WAUME WAWILI MAPYA YAIBUKA; VIPIMO VYA DNA KUMALIZA UTATA WA NANI BABA WA MTOTO.


HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online