Thursday, October 9, 2014

TRAFIKI WA PICHA ZA MAHABA WATIMULIWA KAZI MARA MOJA.

Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani walioachishwa kazi.

ASKARI wa Kikosi cha Usalama Barabarani waliopiga picha ya mahaba wakibusiana huku wakiwa wamevaa sare za Jeshi la Polisi na picha yao ikasambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii wamefukuzwa kazi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe amethibitisha leo kwa waandishi wa habari mkoani humo kuwa, askari hao na mwenzao aliyewapiga picha wametambuliwa na tayari wamefukuzwa kazi kwa kitendo hicho cha kulidhalilisha Jeshi la Polisi.

Kamanda Mwaibambe amewataja askari hao kuwa ni PC Asuma Mpaji Mwasumbi mwenye namba F.7788, PC Fadhiri Linga mwenye namba G 2122 na PC Veronica Nazaremo Mdeme, wote walikuwa askari wa kikosi cha usalama barabarani wilayani Misenyi, mkoani Kagera.

MDEE NA WENZAKE WAPATA DHAMANA BAADA YA KULALA SEGEREA SIKU MOJA.



HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top