Sunday, September 14, 2014

UMEIPATA HII YA WOLPER KUTUMIKA KWENYE UTAPELI WA MAMILIONI; HII HAPA.


 STAA wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper Masawe ‘Jack Wolper’ amejikuta akitumika kwenye utapeli wa mamilioni ya shilingi kupitia mitandao ya kijamii bila yeye kujua,limeinyaka.
Staa wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper Masawe ‘Jack Wolper’

Akizungumzia sakata zima huku alibubujikwa na machozi, Wolper alisema: “Siku moja nilikutana na dereva teksi mmoja aitwaye Ismail, baada ya kupiga stori nilimpa namba yangu ya simu na yeye akanipa yake, tukaagana.

“Siku chache baadaye Ismail akanipigia simu na kuniuliza kulikoni naomba sana watu wanisaidie pesa kwenye WhatsApp kwa ahadi ya kuwarejeshea?“Akaniambia kama nina tatizo bora wakati mwingine nimshirikishe kuliko kila kukicha kuombaomba pesa.

“Hapo ndipo nikagundua kuna mtu kajisajili kwa jina la Jacqueline Masawe na hata kwenye namba nyingine za simu anazotumia kuomba watu pesa, amejisaliji kwa jina hilohilo.“Pia kwenye Facebook, WhatsApp anatumia picha zangu, hapo ndipo nikagundua kuwa, kuna mtu anatapeli watu kupitia jina langu,” alisema Wolper.

Staa wa filamu, ‘Jack Wolper’ akipozi.

Akaongeza kuwa, baada ya kugundua utapeli huo akashangaa wanajitokeza watu wakisema wanamdai ambapo imebainika mtu huyo alikuwa kakopa pesa kwa watu tofauti zinazofikia shilingi milioni 10 lakini wengi walimuelewa hivyo kuripoti tukio hilo kwa vyombo vinavyohusika ili kumsaka mtuhumiwa.

BAADA YA KUMWAGANA NA MFANYABIASHARA WA MADINI; LULU AMNASA MENEJA WA WEMA SEPETU.

TAHADHARI YA MHARIRI
Baadhi ya watu wamekuwa wakitapeli kupitia njia ya mtandao hivyo ni vyema kila mmoja kuwa makini ili kuepukana na matatizo kama yaliyomkuta Wolper.


HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA
PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top