MTOTO Happiness Kashinje (9) (pichani)aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Negezi mjini Shinyanga, ameokotwa akiwa amekufa baada ya kudaiwa kutekwa na watu wasiojulikana kabla ya kubakwa na kutobolewa macho.

Mtoto Happiness Kashinje (9) pichani kulia enzi za uhai wake.
Tukio hilo lilijiri hivi karibuni Nhelegani, Kata ya Kizumbi kilometa chache kutoka nyumbani kwao. Habari zilizofika Uwazi kuhusu mkasa huo zinasema, Happiness aliyekuwa akiishi na shangazi yake, alipotea Agosti 27, mwaka huu baada ya kuaga kuwa anakwenda saluni kupunguza nywele na hakurudi tena hadi siku iliyofuata mwili wake ulipookotwa ukiwa umeanza kuharibika.
Mtuhumiwa huyo alihukumiwa kifungo cha maisha jela. Baadhi ya watoto walioathirika katika matukio ya ubakaji uliofanyika katika maeneo tofauti ya Mji wa Shinyanga walilazwa kwa muda mrefu katika hospitali ya mkoa na wengine kupelekwa Bugando jijini Mwanza lakini hata hivyo, baadhi yao macho yao yameathirika.
TAZAMA PICHA CHAFU ALIZOPIGA HUYU MWANAFUNZI WA CHUO NA BOYFRIEND WAKE KISHA KIZIPOST FB.
Kwa mujibu wa maelezo ya mlezi wa mtoto Happiness, John Njai ambaye ni mume wa shangazi yake, siku moja kabla ya tukio, marehemu aliomba shilingi mia tano kwa ajili ya kunyolea nywele. Baada ya kupewa hela hiyo inadaiwa bibi yake alimtaka anyoe nywele hizo nyumbani ili fedha hiyo itumike kwa matumizi mengine, lakini alikataa kwa madai kuwa angenyolewa vibaya na hivyo kuchekwa na wenzake shuleni.Bibi huyo alimruhusu mjukuu wake kwenda saluni na kwamba akiwa njiani anarudi aliomba lifti kwa watu wawili waliokuwa kwenye baiskeli moja lakini walimnyima kwa madai ya kukosa kiti cha nyuma.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment