Friday, September 5, 2014

LULU AMPA MITONYO MTOTO WA MIL. 50 ZA TMT.

MUIGIZAJI mwenye mvuto wa aina yake katika tasnia ya filamu Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ amempa somo mshindi wa Shindano la Tanzania Move Talent ‘TMT,’ Mwanafaa Mwinzago kuwa asibweteke na ushindi aliopata bali azingatie masomo.

Muigizaji mwenye mvuto wa aina yake katika tasnia ya filamu Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’.
MKE WA KAMANDA BARLOW AFUKUZWA KWA MAPANGA KABURINI KWA MUMEWE!
Akizungumza na Ijumaa juzikati, Lulu alisema ni kweli binti huyo ana kipaji na ilikuwa haki kushinda milioni 50 ila ajue bado ni mtoto na anatakiwa kukomalia elimu.


“Ustaa ni cheo kikubwa sana hasa katika jamii na kila mtu anakuangalia wewe, ili ujikontroo unatakiwa ujitambue na huwezi kujitambua kama huna elimu ya kutosha hivyo mimi namshauri aweke suala la masomo mbele kuliko ustaa alioupata,” alisema Lulu.

Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talent ‘TMT,’ Mwanafaa Mwinzago.

Fainali za TMT zilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Ukumbi wa Mlimani City ambapo Mwanafaa aliibuka kidedea.

HATA KUBONYEZA KA Like Tu Hapo JUU HUTAKI; BONYEZA BASI MPEDWA


PIA ISOME NA HII HAPA CHINI INAKUHUSU

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top