
BAADHI ya akinadada wanaofanya biashara haramu ya kujiuza katika maeneo ya Jiji la Dar, wameeleza kuwa licha ya kupewa kashikashi na jeshi la polisi na wakati mwingine kukamatwa na kupelekwa mahakamani, hawawezi kuiacha ‘kazi’ hiyo kutokana na ugumu wa maisha.
Wadada hao waliyasema hayo, juzi Jumatano baada ya kunaswa na paparazi wetu maeneo ya Sinza Afrikasana pembeni ya Corner Bar ikiwa ni siku chache baada ya baadhi yao kukamatwa na polisi ambapo walisema biashara hiyo ndiyo maisha yao.

Walisema, hawapendi kuifanya lakini wanalazimika kutokana na maisha duni waliyonayo.
“Nani asiyependa kulala usiku na familia yake? Ukituona barabarani ujue hali ni mbaya. Hata kama polisi wanatukamata lakini wanatuachia na tunarudi sokoni kama kawaida,” alisema changu mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Zuena na kuongeza:

“Wateja wetu wenyewe wanajua kuwa hii nguvu ya polisi ni ya soda tu, wakiona tumepigwa ambushi kidogo wanasubiri zipite siku chache kisha tunaendeleza harakati zetu, sisi bila kuja kujiuza hatuwezi kuwasomesha watoto wetu wala kuwalisha.”

“Sasa, achana na mambo ya kutuhoji bwana, tutoe basi kama vipi tukuuzie mambo kwa bei ya ofa. Cheki nilivyojaaliwa,” alisema binti mmoja ambaye ukikutana naye mchana unaweza kusema, ‘mke si ndiyo huyu’.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment