Monday, July 14, 2014

SHILOLE Akataliwa Ukweni na Ndugu za Boyfriend wake wakidai ana Umri Mkubwa kuliko Ndugu yao.


‘Shilole’ akiwa na mpenzi wake ambaye ni msanii wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda
Haijakaa poa! Habari zinadai kwamba baadhi ya ndugu wa msanii wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda ambao ni wakwe wa staa wa muziki na filamu za Kibongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ hawamtaki kwa madai kuwa ana umri mkubwa kuliko ndugu yao.


Staa wa muziki na filamu za Kibongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’

Wakizungumza na Ijumaa Wikienda kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanandugu hao (majina yanahifadhiwa) walisema umri wa Shilole siyo wa kuishi na ndugu yao, Mziwanda kwani hawaendani.
“Ukweli ni kwamba mapenzi hayaingiliwi lakini tunaumia kuona ndugu yetu katika penzi zito na Shilole ambaye hawaendani kiumri,” alidai mmoja wa ndugu hao.

Alipotafutwa Shilole ili kufikishiwa ujumbe wa ndugu hao kwamba hawamtaki, simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa.


Bonyeza Like hapo juu uwe wa kwanza kupata habari mpya.

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top