Tuesday, June 24, 2014

Mwanamke aliyeasi Dini huko Sudan aponea chupu chupu.

 Kwa mujibu wa BBC, Mwanamke wa Sudan aliyehukumiwa kifo kwa kosa la kuikana imani ya dini yake na kuolewa na mwanaume anayempenda wa kikristu amechiwa kutoka gerezani.
Shirika la habari la Suna limeripoti kuwa, hukumu ya kifo iliyotolewa kwa mwanamke huyo Meriam Ibrahim ilibadilishwa na mahakama ya rufaa.

Mwanamke huyo aliolewa na mwanaume wa kikristu na alihukumiwa kifo kwa kutumia sheria za kiislamu Sharia baada ya kukataa kurejea kwenye dini yake.
Mume wake amesema kuwa anatarajia kumuona mke wake akirejea nyumbani.
Aliwekwa gerezani tangu February mwaka huu akiwa na mtoto wake mdogo wa kiume aliyejifungua akiwa ndani.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza

Ungependa stori kama hizi zisikupite na zikufikie wakati wowote? niko tayari kukutumia wakati wowote iwapo utajiunga na mimi kwa kubonyeza Like hapo juu

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top