Wednesday, June 25, 2014

Lupita Nyong’o athibitisha kuwa na uhusiano wa kimapenzi na K’naan

Lupita amezidi kuchukua headlines za vyombo mbalimbali vya habari tangu afanikiwe kuchukua tuzo za Oscar na kutajwa kama mwanamke mrembo zaidi duniani, sasa amethibitisha kuhusu upande wake wa mahusiano kuwa ni kweli ana uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki K’naan kutoka Somalia.


lupita-knaan

Mara ya kwanza Lupita alikuwa akihusishwa na Michael Fassbender na Jared Leto lakini mwigizaji huyo amekita mizizi yake ya kimapenzi kwa rapa K’naan na wanafuraha na mahusiano yao.

Wapenzi hao mara kadhaa wamekuwa wakionekana katika maeneo mbalimbali wakiwa pamoja lakini hawakuwa wakiweka wazi nini kinaendelea kati yao na kufanya watu wahisi tu juu ya uhusiano wao.

lupita_nyongo_vogue_cover

Stori ni kwamba katika jarida la hivi karibuni la Vogue ambalo Lupita ametokea kwenye ukurasa wa mbele amethibitisha kweli ana uhusiano wa kimapenzi na K’naan na anampenda sana.

K’naan ni mzaliwa wa Somalia na ameingia katika umaarufu baada ya kuimba wimbo rasmi wa kombe la dunia kwa mwaka 2010 wa “Wavin’ Flag”.

Ungependa stori kama hizi zisikupite na zikufikie wakati wowote? niko tayari kukutumia wakati wowote iwapo utajiunga na mimi kwa kubonyeza Like hapo juu

Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top