WASANII wawili wa filamu, Nice Mohamed ‘Mtunisi’ na Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ambao walikuwa wapenzi kabla ya kuachana na mwanaume huyo kuoa, sasa wamerudiana rasmi.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho jirani na wasanii hao kimesema wawili hao hivi sasa wanapika na kupakua.Kilisema baada ya kurudiana, kwa sasa wanaishi pamoja kama mume na mke maeneo ya Sinza, jijini Dar es Salaam huku wakiishi kwa amani na upendo.
Hivi karibuni Batuli aliweka picha ya Mtunisi katika akaunti yake kwenye mtandao wa Instagram na kuandika maneno haya “Alichokipanga Mungu hakuna wa kukipangua.”

Nice Mohamed ‘Mtunisi’.
Alipotakiwa kuzungumzia suala hilo, Batuli alisema hawezi kuzungumzia katika vyombo vya habari kwa vile mambo hayo ni maisha yake binafsi.
Kwa upande wake, Mtunisi alicheka na kudai kusikia kutoka kwa watu juu ya mwenzake kuweka picha yake mtandaoni na kuandika maneno ya kimahaba, kitu alichosema hawezi kuzuia nafsi ya mtu kumuweka moyoni.
0 comments:
ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA
Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko PamojaPost a Comment