Thursday, March 13, 2014

Askari wa usalama barabarani alamba kitita cha million 2 kwa kazi nzuri anazofanya.

 Mfanyaakazi wa Idara ya Masoko wa Kampuni ya Vodacom Albert Maneno (wa tatu kushoto) akiongea kabla ya kukabidhi Sh. milioni 2 kwa askari wa kikosi cha Usalama Barabarani Moses Alphage (wa kwanza kushoto) aliyeibuka kidedea katika programu ya kuibua hamasa ya kazi kwa askari hao jijini Dar es salaam iliyoendeshwa na kituo cha Redio Clouds FM. Fedha hizo zimetolewa na wafanyakazi wa Vodacom pamoja na wananchi mbalimbali walioguswa na programu hiyo. Wa kwanza kulia ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova akimkabidhi Askari wa usalama barabarani, Moses Alphage fedha taslimu Sh. milioni 2 zilizochangwa na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania na wasikilizaji wa kituo cha Redio Clouds FM kupitia programu ya kuhamasisha na kupongeza utendaji kazi wa askari wa usalama barabarani jijini Dar es salaam iliyonedeshwa na kituo hicho cha Redio. Alphage huongoza magari katika daraja la Mlalakuwa, Kawe.

Askari wa usalama barabarani, Moses Alphage, akiondoka zake kwa mwendo wa kikakamavu mara baada ya kukabidhiwa cheti na pesa taslimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 2 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova (hayupo pichani).


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova akimkabidhi Askari wa usalama barabarani, Moses Alphage fedha taslimu Sh. milioni 2 zilizochangwa na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania na wasikilizaji wa kituo cha Redio Clouds FM kupitia programu ya kuhamasisha na kupongeza utendaji kazi wa askari wa usalama barabarani jijini Dar es salaam iliyonedeshwa na kituo hicho cha Redio. Alphage huongoza magari katika daraja la Mlalakuwa, Kawe.

Askari wa usalama barabarani, Moses Alphage, akiondoka zake kwa mwendo wa kikakamavu mara baada ya kukabidhiwa cheti na pesa taslimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 2 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova (hayupo pichani).

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova (wa tatu toka kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Askari wa usalama barabarani, Moses Alphage (wa pili kushoto) aliyeibuka kidedea kwenye programu ya kuhamasisha na kupongeza utendaji kazi wa askari wa usalama barabarani jijini Dar es salaam iliyonedeshwa na kituo hicho cha Redio na kujishindia Sh milioni 2. Wa kwanza kushoto ni Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Albert Maneno na kulia ni mtangazaji wa Clouds Said Mohamed maarufu Bonge.
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top