Friday, March 28, 2014

Huyu ndie mtoto wa kitz wa miaka 14 anayetengeza application za simu na kuziuza NOKIA.


Alvin Walter Makundi ni kijana mdogo wa Kitanzania anayeishi na wazazi wake nchini Singapore. Akiwa na umri wa miaka 14 na mwanafunzi wa kidato  cha pili  huko Singapore, tayari ameshatumbukiza jina lake katika orodha ya wataalamu wa application katika moja ya makampuni makubwa duniani ya kutengeneza simu za mkononi ya NOKIA, ambapo anatengeneza applications ambazo  anazituma katika kampuni hiyo ambayo nayo bila hiana huitumia. Kwa idhini ya mama yake. Globu ya Jamii ilipata fursa ya kuongea naye kuhusu hayo maajabu anayoyafanya. Msikilize. hapo chini...


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Bw. Walter P. Makundi, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio Singapore siku alipokutana na kuzungumza nao. Bw. Makundi, ambaye ni Meneja mradi wa kampuni kubwa ya ujenzi ya APCO PTE LTD ya hapo Singapore, ndiye baba mzazi wa Alvin. Kulia kwake ni mkewe, Mama Alvin.
Chini Rais Kikwete akisalimiana na Alvin ambaye aliongozana na mama yake pamoja na dada kuja kumuaga wakati Rais akiondoka Singapore usiku huu.

Msikilize hapa
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top