Friday, February 7, 2014

Jack Chuz awapa makavu wanomshangaa kwa kumaliza mwaka katika ndoa bila kushika ujauzito.

Msanii wa filamu za Kibongo, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ amewapa makavu laivu baadhi ya watu wanaoshangaa na kuhoji inakuwaje anatimiza mwaka mmoja ndani ya ndoa bila kuzaa.



Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ akiwa na mumewe siku ya ndoa yao.
Akizungumzia maneno ambayo amekuwa akiyasikia kutoka hata kwa watu wake wa karibu wakiwemo wasanii wenzake, Jack alisema anawashangaa kwa kuwa wanashindwa kujua kwamba kuolewa ni sheria lakini kuzaa ni majaliwa.

 “Ni kweli ndoa yangu keshokutwa tu inatimiza mwaka mmoja lakini nawashangaa wanaohoji kutokuzaa kwangu, wao wako nje ya ndoa hawajui mambo yanaendaje, wakiingia watajua kuwa kuzaa ni majaliwa ya Mungu,” alisema Jack.
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top