Thursday, April 17, 2014

JOHARI: HARUSI YA RAY NITAKUWA MWANDAAJI CHAKULA.

Mkongwe kwenye sanaa Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’.
 MKONGWE kwenye sanaa Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amefunguka kuwa endapo ikitokea mkurugenzi mwenzake, Vincent Kigos akaoa, yeye atajitolea kuwa mwandaaji wa chakula.

Akizungumza na mwanahabari wetu mwishoni mwa wiki iliyopita, Johari alisema yeye na Ray ni watu wa karibu kwa kuwa wameiongoza kampuni yao kwa muda mrefu hivyo katika jambo muhimu kama la ndoa, lazima ajitoe kinaga ubaga kufanikisha.

Msanii wa Bongo Muvi, Vincent Kigosi 'Ray'.

“Yani hata kama ikitokea kesho mkasikia Ray anaoa ujue kabisa nitakuwa muandazi kuhakikisha madikodiko yanawafikia waalikwa kwa wakati muafaka,” alisema Johari ambaye mara zote amekuwa akikanusha kuwa uhusiano wa kimapenzi na Ray.
Share this article

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top