Sunday, February 2, 2014

Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki, Zanzibar kupatikana leo.


Wananchi Jimbo la Kiembesamaki, Zanzibar wakiangalia majina yao kujua vituo vyao walivyopangiwa kupiga kura leo asubuhi.
 
HABARI kutoka Zanzibar zinasema uchaguzi mdogo wa uwakilishi Jimbo la Kiembesamaki kisiwani humo unaendelea vizuri na wapiga  kura wengi wamejitokeza kwenda kutimiza haki yao ya kimsingi.


Ulinzi umeimarishwa katika vituo vya kupigia kura.
Mwandishi wetu wa huko anasema jana kulikuwa na malumbano ya hapa na pale kwa wanachama wa vyama viwili vikubwa vya siasa, Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na Chama Cha Wananchi (CUF), kwani walikuwa wakitambiana kila upande ukidai utashinda katika kinyang’anyiro cha leo.
Tutakuwa tukiendelea kuwapasha yanayotokea. 
 

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top