Sunday, February 2, 2014

Cheki hapa mapicha ya Jokate alivyom’sapraiz’ Wema On Stage Arusha.

Unaweza kujikuta ukishindwa kuielewa hii hali lakini inabidi ukubaliane na ukweli halisi wa hiki kilichotokea,Jokate na Wema historia yao ilianzia kwenye shindano la kumtafuta Miss Tanzania 2006 ambapo Mshindi alikua ni Wema Sepetu akifatiwa na Jokate kisha mshindi wa tatu akiwa Lissa Jensen.
Headline zilikuja kutengenezwa tena zikiwahusisha warembo hawa kuonekana wako na mtu mmoja ambapo magazeti mengi yaliandika mahusiano haya  yaliyokua yakimhusu Diamond Platnumz kutoka na warembo hawa.
 
Kimepita kimya kirefu sana juu ya hawa watu wawili hadi usiku wa February 01 huko Arusha kwenye Tamasha la Divaz Night Endless Fame ambalo ndani yake kulikua na mastar kadhaa akiwemo Wema Sepetu,Aunt Ezekiel,Martin Kadinda,Kajala,Zamaradi Mketema,Chid Benzi,Mirror,Jordan na wengine kibao.

Tafadhali bofya like kama bado hujabofya kwenye page yetu

 

Wakati Madam Wema Sepetu akimwaga mauno kwenye jukwaa bila kutegemewa na mtu yoyote Jokate alipanda Jukwaani na kuanza kumtunza Wema pesa na wakati huo Wema alikua akicheza Wimbo wa Diamond My Number One ‘Ngololo’ ambapo Jokate aliungana na Wema kuucheza Wimbo huo.

0 comments:

ASANTE KWA KUTEMBEA BLOGU YAKO::KARIBU SANA

Toa Mani yako Hapa usiogope Tuko Pamoja

Post a Comment

 
Copyright © 2014 Chopa News • All Rights Reserved.
| Template Design by Anga Zio Team • Powered by Blogger online
back to top